Kaimu Mkurugenzi Mamlaka ya Usafiri
wa Baharini Zanzibar Abdullah Husein Kombo
Mamlaka ya Usafiri wa Baharini Zanzibar imezifutia rasmi
hati ya kufanya kazi Meli ya Mv.Kalama, Mv.Seagul na Mv.Sepideh kutokana na meli
hizo kutokukidhi hali ya usalama wa abiria katika meli hizo.
Aidha meli hizo zimepewa muda wa mwezi mmoja kuanzia leo
kuhakikisha zimeondoka katika maeneo ya Zanzibar
kabla ya hatua zaidi kuchukuliwa dhidi ya wamiliki wa Meli hizo.
Kauli hiyo imetolewa na Kaimu Mkurugenzi Mamlaka ya Usafiri
wa Baharini Zanzibar Abdullah Husein Kombo wakati alipokuwa akizungumza na
waandishi wa habari Afisini kwake kuhusu hali ya usafiri wa baharini na usalama
Zanzibar. Endelea hapa
No comments:
Post a Comment