Monday, July 30, 2012
Thursday, July 26, 2012
MV KALAMA, MV SEPIDEH NA MV SEAGUL ZAFUTIWA HATI YA KUFANYA KAZI ZANZIBAR
Kaimu Mkurugenzi Mamlaka ya Usafiri
wa Baharini Zanzibar Abdullah Husein Kombo
Mamlaka ya Usafiri wa Baharini Zanzibar imezifutia rasmi
hati ya kufanya kazi Meli ya Mv.Kalama, Mv.Seagul na Mv.Sepideh kutokana na meli
hizo kutokukidhi hali ya usalama wa abiria katika meli hizo.
Aidha meli hizo zimepewa muda wa mwezi mmoja kuanzia leo
kuhakikisha zimeondoka katika maeneo ya Zanzibar
kabla ya hatua zaidi kuchukuliwa dhidi ya wamiliki wa Meli hizo.
Kauli hiyo imetolewa na Kaimu Mkurugenzi Mamlaka ya Usafiri
wa Baharini Zanzibar Abdullah Husein Kombo wakati alipokuwa akizungumza na
waandishi wa habari Afisini kwake kuhusu hali ya usafiri wa baharini na usalama
Zanzibar. Endelea hapa
SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR NA VIKOSI VYA ULINZI NA TAASISI ZA KIRAIA WAPEWA PONGEZI
Makamu wa Pili wa Rais wa
Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akizungumza na Mkuu wa Mabalozi wa Nchi za Nje
waliopo Tanzania Bwana Juma Alfan Mipango hapo Ofisini kwake Baraza la
wawakilishi Mbweni.
Pembani yao ni Balozi wa Umoja wa Falme za Kiarabu {
UAE } Bw.Mallallah Mubarak Alameri.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif
Ali Iddi akizungumza na Meneja Uhusiano
wa Mfuko wa Pencheni wa PPF Bibi Lulu Mengele aliyefika Zanzibar kutoa mkono wa
pole kwa niaba ya Uongozi wa Mfuko huo kufuatia ajali ya meli ya hivi karibuni
karibu na Kisiwa cha chumbe Zanzibar.
Meneja Uhusiano wa Mfuko wa
Pencheni { PPF } Bibi Lulu Mengele akiwasilisha salamu za rambi rambi kwa
Makamu wa PILI WA Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi kufuatia ajali ya Meli
ya M.V.Skagit iliyotokea wiki iliyopita.
Makamu wa Pili wa Rais wa
Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akibadilishana mawazo na Bishop Michael wa Kanisa
la Anglikana Dayosisi ya Zanzibar mara baada ya kuwasilisha salamu zao za rambi
rambi hapo ukumbi wa Baraza la wawakilishi Mbweni.
Pembeni ni Katibu Mkuu wa Dayosisi hiyo Bwana Nuhu
Sallanya.
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa ushirikiano na
Vikosi vya Ulinzi, pamoja na Taasisi za Kiraia imepongezwa kwa hatua iliyochukuwa
katika kukabiliana na Maafa yaliyotokea ya kuzama kwa Meli ya M.V.
Skagit wiki iliyopita.
Pongezi hizo zimetolewa na Uongozi wa Taasisi tofauti
zinazoendelea kutoa mkono wa pole hapa Zanzibar kufuatia vifo vya
watu kadhaa waliokuwemo ndani ya Meli hiyo iliyopata ajali karibu na Kisiwa cha
Chumbe.
Afisa Uhusiano wa Mfuko wa Pencheni { PPF } Bibi Lulu
Mengele Bishop Michael wa Kanisa la
Anglicana Dayosisi ya Zanzibar pamoja na Balozi wa Umoja wa Falme za Kiarabu {
UAE } Bwana Mallallah Mubarak Alameri wakitoa mkono huo wa pole kwa Balozi Seif
walisema hatua hiyo imesaidia kuokoa maisha ya wananchi kadhaa.
Walisema walio wengi wameshuhudia jitihada hizo za
uokozi zilizoleta matumaini ndani ya nyoyo za Jamii.
Hata hivyo wawakilishi hao wa taaasisi tofauti
walisema licha ya juhudi hizo za Serikali lakini bado ipo haja ya msingi ya
kufuatwa kwa sheria na Taratibu sa usafiri wa Baharini.
Walisema utaratibu huo mbali ya kupunguza zinazoweza
kuepukwa lakini pia utasaidia kuondosha mwanya kwa Wafanyabiashara na
Wawekezaji wakorofi wanaoendesha biashara hiyo ya vyombo vya usafiri wa
Baharini.
“ Kitu cha msingi ni kufuatwa kwa sheria na taratibu
za usafiri nah ii itaondosha uzembe na ujanja unaotumiwa na wafanyabiashara
wakorofi”. Alisisitiza Balozi wa UAE Bwana Mallallah.
Naye kwa upande wake Bishop Michael wa Kanisa la
Anglikana la Mkunazini Dayosisi ya Zanzibar
amesema hatua za serikali za kurejesha hali ya amani kufuatia fujo za baadhi ya Vijana zilizofanywa hivi karibuni
imeleta faraja kwa waumini wa kanila lao.
Bishop Michael alisema Uongozi wa Kanisa hilo utaendelea
kuwaelimisha Waumini wao kulinda na kuheshimu amani ya Taifa ambayo inahitajiwa
na kila mwana Jamii.
Akitoa shukrani zake Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali
Iddi alisema Viongozi wa Serikali wanaendelea kupata matumaini kuona Taasisi na
mshirika mbali mbali ndani na nje ya Nchi yanaunga mkono juhudi za Serikali.
Balozi Seif alisema Serikali kwa upande wake
itaendelea kuchukuwa hatua madhubuti ili kuzuia majanga yanayoweza kuwepukwa
ambayo yamo ndani ya uwezo wa mwanaadamu.
“ Tumeanza kuchukuwa hatua za kukabiliana na hali hii
kwa kuwaomba washirika wetu ndani na nje ya Nchi kutusaidia katika sekta hii Likiwemo
hili zito la upatikanaji wa meli kubwa ya usafirishaji wa wabiria na mizigo”.
Alifafanua Balozi Seif.
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
26/7/2012.
SWAUMU YA LEO IMO!!!
Mariam Hamza mtoto wa pili wa bi Hamida Maalim alipokuja kutembelea Coconut Fm leo
Mariam
Hamida Maalim nikiwa na Mama wa mitaani Aisha Omary kushoto tukibadidlishana mawazo kuhusu mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Wednesday, July 25, 2012
RAMADHANI KAREEM.....JAMILA ABDALAH
Mwanamke kujistiri huu ndio muonekano wa Baby J kwa mwezi huu mtukufu wa Ramadhani tofauti na vile watu walivyomzoea kwa muonekano wa kawaida.
Friday, July 20, 2012
RAISI WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI DR ALI MOHAMED SHEIN AWASISITIZA WAISLAM KUWA WATUMIAJI WAZURI WA MISKITI
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein, amewasisitiza Waumini wa dini ya Kislamu kutoitumia misikiti kuwa vivutio vya kusababisha uhasama, malumbano au kuwafarakanisha waumini na watu wengine.
Alhaj Dk. Shein aliyasema hayo katika ufunguzi wa msikiti wa Rahmatullah uliopo Mwanyanya, Wilaya ya Magharibi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, ambapo viomngozi mbali mbali wa dini, vyama na serikali walihudhuria akiwemo Rais mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Alhaj Ali Hassan Mwinyi.
Katika hotuba yake Dk. Shein alieleza kuwa misikiti iwe kwa ajili ya ibada pamoja na kuendeleza elemu miongoni mwa waislamu.
Alhaj Dk. Shein aliyasema hayo katika ufunguzi wa msikiti wa Rahmatullah uliopo Mwanyanya, Wilaya ya Magharibi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, ambapo viomngozi mbali mbali wa dini, vyama na serikali walihudhuria akiwemo Rais mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Alhaj Ali Hassan Mwinyi.
Katika hotuba yake Dk. Shein alieleza kuwa misikiti iwe kwa ajili ya ibada pamoja na kuendeleza elemu miongoni mwa waislamu.
KARIBU MGENI WETU RAMADHANI TWAKUKARIBISHA KWA FURAHA NA AMANI SISI KRUU NZIMA YA COCONUT FM KWA PAMOJA AMIN RABIL ALAMINA..
Meneja wa Coconut Fm ambae pia ni mtangazaji wa kipindi cha Nipe Nikupe akiwa katika pozi muda mfupi baada ya kuzungumza na watangazaji wake.
Juu na chini ni picha ya pamoja ya watangazaji wa Coconut fm
Coconut fm yajipanga kufanya vipindi vizuru vitakavyoendana na mwezi
mtukufu wa Ramadhani ikiwa ni siku chache zimebaki kuweza kuupokea mwezi
huo mtukufu.Meneja wa Coconut Fm Husna Abdul Megeni wa Bahari alisema "Coconut fm ni redio inayomhudumia vizuri mzanzibari katika kupata taarifa muhimu za ndani na nje na kwa upande wa burudani pia hivyo kuna umuhimu mkubwa wa kuendelea kumpatia huduma nzuri zaidi kwa mwezi huu mtukufu wa Ramadhani" aliyaesema hayo jana alipokuwa akizungumza na watangazaji wa Coconut fm na kusisitiza kuwa vipindi vimepangwa vizuri kulingana na mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Pia amewataka wasikilizaji wa Coconut fm kuendelea kusikiliza vipindi vizuri vilivyondaliwa kwa ajili ya mwezi mtukufu na kuwahakikishia kuendelea kutoa huduma bora itayokidhi haja yake kwa kipindi chote.
Kwa upande wa wafanyakazi na waendeshaji wa vipindi wamesema wamefurahishwa sana na mpangilio wa vipindi walioupanga kwa ajili ya Ramadhani.
Thursday, July 12, 2012
Hapo tulipo ni maeneo ya nyuma ya steji kabla Daimond plet nam hajaanza shoo.
hao ni densaz wa plet nam msafi nikishoo nao kabla hajaoyesha vitu vyao.
Jamanii mtoto nilifurahije na vijanaa adi raha yani ful mafuraha yaniiiii.
Aiseeee ni nomaaaa kijana Sultani kingi mtoto kutoka jupiter jinsi alivyo fanya vituuuz
Hapo kijana daimond plet na msafiiii akitoka jasho baada ya kufanya vitu vya hatarii stejini yani we acha tu
Ni tamasha la kumi na tano la ziff ambalo linaendelea nchini Zanzibar na limepokelewa vizuri sana na wananchi wa Zanzibar, katika tamasha hilo kijana ambae anafanya vizuri sana hapa nchini Tanzania katika muziki wa bongo fleva ,Daimond plet nam msafiii alipata nafasi ya kuwa burudisha wananchi wa zanzibar na wageni (watalii) kabla ya kwenda stejini Daimondi alipata nafasi ya kufanya mahojiano coconut fm na mtangazaji wa run the beat Yoram shoo tano, kikubwa alicho ahidi ni kufanya shoo moja kali sana,na baada ya kutinga katika steji kitu ambacho alikifanya huwezi amni, alifanya shoo moja kali sana alitisha mbayaaaa.
Mbali na Daimond, kijana kutoka zanzibar Sultani king alifanya shoo ambayo hakuna mtu aliyetarajia kwa kupafom live.
Mbali na Daimond, kijana kutoka zanzibar Sultani king alifanya shoo ambayo hakuna mtu aliyetarajia kwa kupafom live.
Wednesday, July 11, 2012
KARIBUNI WAGENI WETU
Tumepokea wageni wageni 7 leo kutoka chuo cha uandishi wa habari na utangazaji Zanzibar na 1 kutoka DSJ, tunafuraha kubwa ya kupata ugeni huo ambao watakuwepo kwa muda wa miezi 2 kwa ajili ya kujifunza kwa vitendo.
Katika picha ya juu kutoka kushoto ni Said Mohammed kutoka Zjmmc, Saada Khamis kutoka Zjmmc, Mastura Maulid kutoka Zjmmc, Rehema Khamis kutoka DSJ, Mwakaje Khamis kutoka Zjmmc na mwisho ni Rehema Makame kutoka Zjmmc.....endelea hapa
Katika picha ya juu kutoka kushoto ni Said Mohammed kutoka Zjmmc, Saada Khamis kutoka Zjmmc, Mastura Maulid kutoka Zjmmc, Rehema Khamis kutoka DSJ, Mwakaje Khamis kutoka Zjmmc na mwisho ni Rehema Makame kutoka Zjmmc.....endelea hapa
Sunday, July 1, 2012
MIE NIKIWA KATIKA KIPINDI CHA MAMBO YA ZENJI LEO
Hapa unapo niona nilikua nikipitia sms ya msikilizaji wangu wa mambo ya zenji
Na hapo pia nilikua nikipitia sms ambazo zilitumwa kupitia sm yangu ya mkononi
Maranyingi umezoea kunisikia siku ya jumamosi katika Rusharoho Kitchen part kila siku za juma mosi, lakini leo ilikuwa ni suprise kwako kunisikia katika Mambo ya Zenji kuanzia saa 12 jioni mpaka saa 3 za usiku,
Nimekupasha ishu ya Mwanahawa ali na mama wa mipasho nchini Tanzania na Malkia wa mipasho Khadija Omari Kopa kuwa jukwaa moja kesho nitakupasha zaidi.
Ashura Machupa kutoka katika kundi la mashauzi classic na kuamua kuimbia zing zong, na nilimuuliza swali katika kipindi cha kitchen part kwanini aliamua kutoka katika bendi hiyo ya Isha,alicho jibu nikwamba maslai ni madogo ndipo akaamua kutoka,lakini mengi zaidi tembelea blog hiii uta pata na pia endelea kusikiliza rusha roho kitchen part kila jumamosi.
Subscribe to:
Posts (Atom)